Madereva  wa  bodaboda licha ya biashara ya kusafirisha abiria, wamezua 
tabia nyingine ya kufanya ngono na  wateja wao wa kike, hasa wanafunzi 
na wake za watu.
Imebainika kuwa baadhi ya madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda 
wanatumia usafiri huo kuwarubuni na kuwashawishi wanafunzi wa kike wa 
shule za msingi na sekondari na kufanya nao ngono.
Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi Jumapili jijini Dar es Salaam katika 
Wilaya za Temeke, Ilala na Kinondononi, umebaini kuwa wanafunzi wengi 
wamejiingiza katika vitendo vya ngono baada ya kunaswa na ulaghai wa 
madreva bodaboda wengi wakiwa vijana wadogo.
Madereva hao wamekuwa wakifanya ngono na wanafunzi, baada ya kuahidi 
kuwasafirisha bure kwenda na kurudi kutoka shuleni, hasa kwa maeneo 
ambayo hakuna usafiri wa daladala au eneo lililo mbali na kituo cha basi
 wakati wa kutoka au kwenda shuleni.
Gazeti hili limebaini kwamba, baadhi ya walimu pia wamejiingiza katika 
mchezo huo mchafu na kufanya ngono na vijana wadogo wanaoendesha 
bodaboda.
Madereva hao wanaoonekana katika vituo vya daladala, huwafuata wanafunzi
 hao wanaosumbuliwa na shida ya usafiri wakikataliwa kupanda daladala 
makondakta wa daladala hasa wakati wa asubuhi na jioni.
 
 

 
No comments:
Post a Comment