Tamko
 hilo lilitolewa jijiji Mbeya na Mkurugenzi wa Sheria na Leseni wa 
mamlaka hiyo, Elizabeth Nziga wakati wa semina kuhusu utekelezaji wa 
sheria mpya ya mawasiliano ya elektroniki na posta ya mwaka 2010 kwa 
wadau mbalimbali.
Hiyo
 ni awamu nyingine katika mipango ya TCRA, kwani awali ilikuwa na 
kampeni za kuzima mitambo ya analogia nchi nzima na kuwataka wananchi 
kuingia katika mfumo wa dijitali ulioanzia katika Mkoa wa Dar es Salaam 
Desemba 31, mwaka jana.
Mikoa
 mingine iliyoingia kwenye mfumo wa dijitali ni Arusha, Tanga, Dodoma, 
Mbeya na Mwanza. Nziga alisema mamlaka hiyo inasisitiza kuwa hatua hiyo 
ni utekelezaji wa makubaliano kati yake na watoa huduma za mawasilino ya
 simu na kufikia usiku wa Juni Mosi, namba za simu ambazo hazikusajiliwa
 zitakoma. Mmiliki wake hataweza kuitumia kupiga wala kupokea siku.
 
 
 
 
 





